
Taarifa ya kushtua ambayo imeripotiwa na majukwaa mbalimbali ya mitandao ya kijamii na kuthibitishwa na uongozi wa Yanga zimeeleza kuwa kocha mkuu wa Yanga, Sead Ramovic amefikia makubaliano ya pande mbili ya kuachana na timu hiyo, huku ikielezwa yupo kwenye rada za kutua nchini Algeria kwenye klabu ya CR Belouzdad.
Ikumbukwe Ramovic alichukua jukumu la kuiongoza Yanga mwezi Novemba mwaka jana 2014 na hii ni mara baada ya kuondoka kwa aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho Muargentina, Miguel Gamondi.
Kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya kocha mkuu mpya, Miloud Hamdi mwenye asili ya nchini Argentina na Ufaransa.
This is nicely said! !