By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Geita yafikia 95% utekelezaji wa ilani ya CCM
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Uncategorized

Geita yafikia 95% utekelezaji wa ilani ya CCM

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa kwenye kikao Cha baraza la madiniwani
Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 9:27 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

HALMASHAURI ya wilaya ya Geita mkoani hapa imeweka wazi kuwa mpaka kufikia Februari 2025 tayari imefikia asilimia 95 ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020-2025.

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, Khadija Said amesema hayo katika mkutano wa Baraza la Madiwani kwa Kipindi cha Robo ya Pili kwa mwaka wa Fedha 2024/25.

Amesema mafanikio hayo ni matokeo ya ushirikiano kati ya madiwani, viongozi na maofisa wa halmashauri ambapo kila mmoja kwa nafasi yake amewajibika kikamirifu kutatua kero za wananchi.

Amesema kupitia fedha zinazotolewa na serikali ya awamu ya sita halmashauri imesimamia kwa uafasaha kuhakikisha kila kata, kijiji na kitongoji kinapata huduma muhimu za kijamii hususani maji, afya na elimu.

“Kama kuna diwani ambaye ameshindwa kutekeleza ahadi alizotoa kwenye kata yake, nitoe wito kwa madiwani wenzangu waendelee kukumbuka zile ahadi alizotoa ili waweze kuondoa adha za wananchi”, amesema.

Diwani wa Kata ya Bukoli, Faraji Self amesema kwa upande wa kata hiyo utekelezaji wa ilani umefikia asilimia 93 na juhudi kubwa zinafanyika ili kukamilisha asilimia 100 kabla ya kuvunjwa kwa bunge.

Faraji amedokeza miradi inayoendelea ni ujenzi wa jengo la upasuaji, jengo la zahanati na maabara katika kijiji cha Ntono pamoja na shule mpya ya sekondari.

“Changamoto kubwa iliyopo ni mfumo wa NEST, ambao ndio unatusumbua lakini watendaji tunawapongeza kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya kwenye miradi hii hakuna hujuma”, amesema

Diwani wa kata ya Busanda, Seleman Gamala amesema ndani ya miaka minne kata hiyo imepokea zaidi ya sh billioni mbili kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali sambamba na pesa za mfuko wa jimbo.

“Kata ya Busanda mfuko wa jimbo umetunufaisha sana, tumepokea zaidi ya sh milioni 22 kwa ajili ya ujenzi wa daraja, ofisi za kijiji, mara ya kwanza tulipokea milioni 18, mara ya pili tukapata milioni nne.

Mhe. Khadija Saidi Makamu mwenyekiti wa baraza la madiwani Wilaya ya Geita
Diwani wa Kata ya Bukoli, Faraji Self, akizungumza na Waandishi wa Habari kando mwa kikao hicho
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita wakiwa kwenye kikao Cha baraza la madiniwani

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

The Biggest Hollywood Celebrities Visit the Jungles of Thailand

The Best Pork Kebabs With Grilled Plums and Couscous is Found in Poland

Hakikisheni CCM inaendelea kutawala – Dk. Mwinyi

Exploring Extracurricular Opportunities for Student

Kristen Stewart Was Seen Having Lunch in Toronto with Boyfriend

Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Hakikisheni elimu ya malezi inaifikia jamii kikamilifu – Theresia Ngonyani
Next Article Uzinduzi wa jengo la hazina Mkoani Geita
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version