By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Mhe. Kanyasu atimiza ahadi ya pikipiki kwa wanahabari Geita
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Mhe. Kanyasu atimiza ahadi ya pikipiki kwa wanahabari Geita

Gharos Riwa, Geita
Last updated: March 1, 2025 10:56 am
Gharos Riwa, Geita
3 months ago
Share
SHARE

Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, ametekeleza ahadi yake kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Geita (GPC) kwa kukabidhi pikipiki tatu zitakazorahisisha kazi za uandishi wa habari katika mkoa huo.

Katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika leo, Mheshimiwa Kanyasu amepongeza juhudi za waandishi wa habari katika kuhabarisha na kuelimisha jamii, akisema kuwa mchango wao ni muhimu kwa maendeleo ya taifa.

“Ninatambua kazi kubwa inayofanywa na waandishi wa habari katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kwa wakati. Pikipiki hizi zitawasaidia kuwafikia wananchi kwa haraka na kufanya kazi yenu kwa ufanisi zaidi,” alisema Mheshimiwa Kanyasu.

Mwenyekiti wa GPC, Bw. Renatus Masuguliko, amepongeza juhudi za Mbunge huyo na kueleza kuwa msaada huo utakuwa chachu ya kuboresha mazingira ya kazi kwa wanahabari wa Geita.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Kanyasu kwa kutimiza ahadi yake. Pikipiki hizi zitatuwezesha kufuatilia matukio kwa wakati na kuhakikisha habari zinawafikia wananchi haraka,” alisema Bw. Masuguliko.

Hafla hiyo imehudhuriwa na waandishi wa habari wa Geita pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya habari, ambao wamesisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana katika kuboresha mazingira ya kazi kwa wanahabari nchini.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

Hakikisheni elimu ya malezi inaifikia jamii kikamilifu – Theresia Ngonyani

UCHUNGUZI WA VURUGU SHULE YA SEKONDARI YA GEITA, WANAFUNZI 71 WACHUKULIWA HATUA

NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA

Wawili wafariki dunia ajali ya basi Geita

TAGGED:MbungeWanahabari
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka
Next Article UCHUNGUZI WA VURUGU SHULE YA SEKONDARI YA GEITA, WANAFUNZI 71 WACHUKULIWA HATUA
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version