By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi

Katibu Tawala Wilaya ya Chato. Ndg Thomas Dime,
Gharos Riwa, Geita
Last updated: March 1, 2025 10:42 am
Gharos Riwa, Geita
3 months ago
Share
SHARE

Serikali katika wilaya ya chato Mkoani Geita imewaomba wadau wa elimu kuendelea kushirikiana na serikali ili kutatua upungufu wa madawati kwa wanafunzi wa shule za Msingi na sekondari wilayani humo.

Rai hiyo imetolewa na katibu tawala wilaya ya Chato Thomas Dime wakati akimwakilisha mkuu wa wilaya hiyo katika hafla ya kukabidhi madawati, viti pamoja na vifaa tiba kwenye shule ya Msingi Mkuyuni vilivyotolewa na benki ya Nmb katika wilaya hiyo vilivyotolewa kwa lengo la kutatua changamoto katika sekta ya elimu pamoja na afya.

Dime amesema wilaya ya Chato inakabiliwa na upungufu wa madawati zaidi ya elfu 26 kwa shule za Msingi pamoja na elfu 6 kwa shule za sekondari na kuwaomba wadau wa elimu, serikali kupitia Halmashauri pamoja na wananchi kushirikiana kutatua tatizo hilo.

Meneja wa benki ya Nmb kanda ya ziwa Faraja Raphael Ng’ingo amevitaja vifaa hivyo vilivyotolewa na benki hiyo vimegharimu kiasi cha shilingi Milioni 29.5 na vitainufaisha hospitali ya Rufaa kanda ya Chato, shule ya Rubambagwe, Itale, Lumasi pamoja na shule ya Msingi Mkuyuni.

Mbunge wa jimbo la Chato Dk. Medard Matogoro Kalemani na Mwenyekiti wa kijiji cha Mkuyuni cha Mkuyuni Goodluck Phinias wameishukuru benki ya Nmb kwa msaada wake na kuomba kuendelea kujitoa katika kuchochea maendeleo ya wilaya ya Chato katika nyanja mbalimbali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali Wilaya ya Chato kupitia kwa katibu tawala wa wilaya hiyo Thomas Dime inaeleza kuwa wilaya hiyo kwa kushirikiana na wakala wa misitu TFS wamepanga kutumia misitu iliyopo kutengeneza viti na meza kukabiliana na tatizo hilo .

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao

Wanafamilia washikiliwa na Polisi wakituhumiwa kuua baba yao mzazi

Uzinduzi wa jengo la hazina Mkoani Geita

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Mhe. Kanyasu atimiza ahadi ya pikipiki kwa wanahabari Geita

TAGGED:Elimu ya MsingiGeita
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Wawili wafariki dunia ajali ya basi Geita
Next Article Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi saidieni kutatua kero za walimu
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version