By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi saidieni kutatua kero za walimu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Uncategorized

Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi saidieni kutatua kero za walimu

Gharos Riwa, Geita
Last updated: February 28, 2025 9:03 am
Gharos Riwa, Geita
3 months ago
Share
SHARE

Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote Nchini wametakiwa kuanzisha kliniki ndogondogo za walimu ili kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili.

Rai hiyo imetolewa, Februari 26, 2025, na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Mashaka Biteko, wakati wa kliniki ya kusikiliza na kutatua kero za Walimu iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu, Manispaa ya Geita.

Dkt. Biteko amesema kuwa baadhi ya changamoto za walimu zinaweza kutatuliwa katika ngazi za halmashauri bila kufikishwa kwenye ngazi za juu za serikali, endapo tu walimu watawasilisha kero zao kwa wakati kupitia viongozi wao wa halmashauri.

Akizungumzia mafanikio ya sekta ya elimu katika serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Dkt. Biteko amesema kuwa zaidi ya walimu 10,839 wamepandishwa madaraja, huku shilingi bilioni 4.6 zikitumika kuwalipa madeni na malimbikizo ya mishahara walimu 5,061. Aidha, walimu 876 wamebadilishiwa muundo wa ajira baada ya kujiendeleza kielimu.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya sita inatambua na kuthamini mchango wa walimu katika maendeleo ya sekta ya elimu, ambapo shilingi milioni 25 zimetumika kwa ajili ya matibabu ya walimu katika Mkoa wa Geita kwa mwaka 2024.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Paschal Katambi, amesema serikali imefanya mabadiliko katika sera na sheria za utumishi wa umma, ikiwemo sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii PSSF na NSSF, ili kuendana na mahitaji ya sasa na kuondoa kero zinazowakabili watumishi, wakiwemo walimu.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martin Shigela, amepongeza Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kubuni mbinu bora za kutatua kero za walimu kwa kuwakutanisha na serikali.

Kliniki hiyo imeratibiwa na CWT kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora, Wizara ya Fedha, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC-HQ).

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Uzinduzi wa jengo la hazina Mkoani Geita

The Biggest Hollywood Celebrities Visit the Jungles of Thailand

Hakikisheni CCM inaendelea kutawala – Dk. Mwinyi

Video ya mabinti wanaompigania Mwijaku yatua mezani kwa Mhe. Gwajima

Best Places to Get Your Mexican Food Fix When You Visit Mexico City

TAGGED:DCsGeitaWalimu
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi
Next Article Dk. Kalemani – Sauti ya Wanawake ni Sauti ya Mungu
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version