By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Dar msisubiri mwishoni kujiandikisha daftari la wapigakura
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
KitaifaMikoani

Dar msisubiri mwishoni kujiandikisha daftari la wapigakura

Mwandishi Wetu
Last updated: March 20, 2025 11:34 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

WAKAZI wa Dar es Salaam wameanza kujiandikisha na wengine kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Mchakato huo ulianza Jumatatu huku Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ikihimiza wananchi waendelee kujitokeza.

Tunaipongeza serikali kupitia INEC kwa uratibu na usimamizi thabiti wa mchakato huu ambao umeshakamilika katika mikoa 29 na sasa ipo kwenye mzunguko wa mwisho Dar es Salaam pekee.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele, sasa wapo katika mzunguko wa 13.

Mchakato huu, ulioanza Dar es Salaam Jumatatu, ukitarajiwa kukamilika Machi 23, 2025 ni sehemu muhimu ya demokrasia nchini ukitoa fursa muhimu kwa kila Mtanzania kuhakikisha kuwa anajiweka sawa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Uandikishaji au uboreshaji wa daftari hili ni jukumu muhimu kwa kila mwananchi anayekidhi vigezo kushiriki.

Hivyo, hatuna budi kuungana na INEC kuhimiza wakazi wa Dar es Salaam kutumia siku hizo zilizopangwa kukamilisha kazi hiyo.

Hata hivyo, kumekuwapo na utamaduni uliojengeka katika jamii, ambapo baadhi ya watu hujisahau kushiriki masuala kama haya siku za mwanzoni badala yake husubiri hadi siku za mwishoni.

Huu ni utamaduni mbaya ambao jamii haina budi kuondokana nao hususani kipindi hiki cha uandikishaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Kwa wananchi wasio na sababu muhimu za kusubiri, wawahi wakajiandikishe ili kuepusha misururu isiyo ya lazima katika siku za mwishoni. Hali hiyo mara nyingi husababisha malalamiko mengi kuhusu huduma.

Tunapenda kuwahimiza wakazi wote wa Dar es Salaam kujitokeza mapema ili kushiriki katika mchakato huu wenye manufaa makubwa kwa taifa na watu wake.

Kuboresha au kujiandikisha katika daftari hilo la mpigakura ni haki ya kila Mtanzania anayekidhi vigezo ajitokeze
katika vituo vilivyopangwa aipate.

Izingatiwe kwamba serikali imetenga rasilimali nyingi kwa ajili ya mchakato huu. Kwa hiyo, ni wajibu wa kila mwananchi kuunga mkono mchakato huu wa kidemokrasia.

Rai yetu kwa wakazi wa Dar es Salaam ni kwamba wahimizane kujiandikisha mapema ili kuepuka msongamano
baadaye. Hii ni fursa adhimu.

Mchakato huu uchukuliwe kwa uzito ili matarajio ya INEC yatimie; ya kuandikisha wapigakura wapya 643,420 mkoani Dar es Salaam ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 18.7 ya 3,427,917 waliopo kwenye daftari la kudumu la wapigakura.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

DKT. BITEKO: Wakristo liombeeni Taifa

Umeme kila mahali ni ndoto ya Rais Samia

CHADEMA: Tundu Lissu yuko Ukonga, nendeni mkamuone

Biteko akemea ubabe Tanesco, ataka hatua

TAGGED:DarDar es SalaamKujiandikishaKura
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Halotel wazindua huduma kukabili matapeli mitandaoni
Next Article Hongera Dkt. Samia Suluhu Hassan, umeweza, tusonge mbele
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version