By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
KitaifaMikoani

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Mwandishi Wetu
Last updated: March 23, 2025 8:34 pm
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu limekanusha madai kuwa gari lake lilitumika kubeba wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mnamo Machi 22, 2025, kama ilivyosambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo, gari la polisi lenye namba PT.4342 lilikuwa likitoka Wilaya ya Itilima kuelekea Bariadi kwa kazi maalum. Katika Kijiji cha Budalabujiga, askari walilikuta gari jingine lenye namba T.356 AAK, mali ya Kampuni ya Allince, likiwa limeharibika.

Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Itilima, aliyekuwa kwenye gari hilo la polisi, aliamuru kusimamisha ili kufahamu hali ya abiria waliokuwa kwenye gari lililoharibika. Wananchi waliokuwa kwenye gari hilo walieleza kuwa walikuwa wakisafiri kuelekea Bariadi na waliomba msaada wa usafiri kutokana na hali mbaya ya hewa iliyosababishwa na mvua

Kutokana na hali hiyo, na kwa kuzingatia wajibu wa Jeshi la Polisi wa kulinda usalama wa raia na mali zao, Mkuu wa Upelelezi aliruhusu wananchi hao kupanda gari la polisi na kuwafikisha Bariadi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu limeeleza kuwa kitendo hicho kilikuwa ni msaada wa kibinadamu na si kubeba wanachama wa chama chochote cha siasa kama inavyodaiwa kwenye mitandao ya kijamii. Polisi wamewataka wananchi kuzingatia ukweli na kuepuka kusambaza taarifa zisizo sahihi zinazoweza kuchochea taharuki.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Kusitishwa ufadhili wa Marekani na hatma ya Wafanyakazi wa mashirika Tanzania

DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka

Hamasisheni Uwekezaji Mtwara – Dk. Hussein

Ofisi ya Makamu wa Rais yapongezwa

Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili

TAGGED:CCMPolisiSimiyu
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili
Next Article Jaji alipohukumu wasikilizaji wa kesi kumlipa fidia mtoto maskini
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version