By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
KitaifaMikoani

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

Mwandishi Wetu
Last updated: April 4, 2025 11:32 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameviagiza vyombo vya usalama barabarani nchini kuongeza nguvu katika usimamizi wa sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kuwafutia leseni madereva wote wanaosababisha ajali za barabarani zinazopelekea vifo, ili kupunguza na hatimaye kutokomeza kabisa wimbi la ajali nchini.

Dkt. Samia ametoa agizo hilo wakati akitoa salamu za pole kufuatia tukio la ajali ya barabarani liyotokea Aprili 3, 2025 na kuhusisha basi la abiria mali ya kampuni ya Mvungi, lililokuwa likitoka Ugweno wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, kuelekea Dar es Salaam.

Ajali hiyo ilipelekea vifo vya watu nane huku wengine 41 wakijeruhiwa ambapo inaelezwa kwamba ilitokana na basi hilo kuacha njia ilipokuwa inapishana na gari ndogo na hatimaye kuserereka kwenye mlima katika eneo la Kikweni, kata ya Msangeni wilayani humo.

Mbali ya maelekezo hayo kwa vyombo vinavyohusika na usimamizi wa usalama barabarani nchini, Dkt. Samia pia amewataka watumiaji wote wa barabara kuhakikisha wanakuwa waangalifu na kufuata sheria za usalama barabarani ili kupunguza majanga ya ajali yanayosababisha vifo na majeruhi wengi kila mwaka.

Akiongea na mwandishi wa habari hizi kuhusu agizo hilo la Dkt. Samia, Irene Msellem ambaye ni balozi wa usalama barabarani kupitia shirika la RSA Tanzania amesema

“Ni hatua ambayo itasaidia sana ikiwa itatekelezwa na wasimamizi wa sheria, sote tunafahamu kwamba ajali nyingi zinatokana na uzembe wa watumia barabara hususan madereva ambao makosa mengi wanayofanya yanayo sababisha ajali ni yenye kujirudia rudia, hii ikimaanisha adhabu za faini haziwafanyi wajutie na kujifunza hivyo hili la kufungiwa leseni linaweza kusaidia wakabadilika haraka zaidi”

Aidha, balozi Irene amewaomba Watanzania kufahamu kwamba ajali nyingi zinaweza kuepukika ikiwa watumia barabara hususan abiria kwenye vyombo vya moto watatimiza wajibu wao mkubwa ambao ni kuelimisha, kukemea na kuripoti matukio yote ya barabarani wanayoona yanafanywa na madereva yakihatarisha usalama wao au wa watumiaji wengine wa barabara

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Mbunifu wa jina la TANZANIA afariki dunia akiwa Uingereza

Uzinduzi wa jengo la hazina Mkoani Geita

Hamasisheni Uwekezaji Mtwara – Dk. Hussein

AJALI ZA BARABARANI ZINACHANGIA ASILIMIA 55 YA WANAOLIPWA FIDIA WCF

Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2

TAGGED:AjaliDkt SamiaKilimanjaroMaderevaPolisi
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Simba waja na kaulimbiu ya HII TUNAVUKA mahususi kwa Al Masry
Next Article RC Dar: Usalama Dar ni shwari, Ujenzi Jangwani mboini kuanza
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version