By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Daraja la Magufuli kuanza kutumika Aprili 30
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kitaifa

Daraja la Magufuli kuanza kutumika Aprili 30

Mwandishi Wetu
Last updated: March 23, 2025 2:09 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Dkt. Charles Msonde amesema daraja la J.P Magufuli (Kigongo Busisi)KM 3 litaanza kutumika rasmi Aprili 30 mwaka huu.

Hata hivyo, amesema ifikapo Aprili 10, 2025 magari yataanza kupita upande mmoja kwenye daraja hilo ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 97.

Daraja hilo limejengwa kwa lengo la kuunganisha Barabara Kuu ya Usagara – Sengerema Geita KM90 ambayo ni sehemu ya barabara iliyopo kwenye Ushoroba wa Ziwa Victoria inayoanzia Sirari mpakani mwa Tanzania na Kenya hadi Mutukula mpakani mwa Tanzania na Uganda.

Kwa sasa sehemu ya barabara hiyo eneo la Kigongo Busisi inaunganishwa kwa kutumia vivuko vikubwa vitatu vya MV Mwanza, MV Misungwi na MV Sengerema.

“Kutokana na idadi kubwa ya magari yanayopita kwa siku, abiria na magari huweza kutumia muda wa takriban saa mbilii kuvuka kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine hivyo kukamilika kwake kutachochea maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza” amesisitiza Dkt. Msonde.

Amesema baada ya daraja hilo kukamilika, muda wa kuvuka utapungua kufikia wastani wa dakika tatu (3) hadi nne (4) badala ya saa mbili ilivyo sasa.

Akizungumza leo Machi 22, 2025 wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma(PIC) ilipokagua ujenzi wa daraja hilo, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Msonde amesema Aprili 10, mwaka huu magari yataruhusiwa kuanza kupita kwenye upande mmoja wa daraja ambao utakuwa umekamilika kwa asilimia 100.

Daraja hilo lenye urefu wa kilomita 3 na upana wa meta 28.45 lina njia mbili za magari zenye upana wa mita 7 kila upande.

Dkt. Msonde amesema daraja hilo ambalo ujenzi wake umegharimu zaidi Shilingi ya bilioni 610 uimefikia asilimia 97.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma, Augustine Vuma Holle ameipongeza Wizara ya ujenzi na Wakala wa Barabara (TANROADS) kwa kazi waliyoifanya kwenye daraja hilo, huku Kamati hiyo ikibainisha ni miongoni mwa miradi bora iliyoridhisha katika ukaguzi wa kamati hiyo.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Watu 7 wapoteza maisha ajali ya ambulance na toyo wilayani Mafinga

Mbunifu wa jina la TANZANIA afariki dunia akiwa Uingereza

Kusitishwa ufadhili wa Marekani na hatma ya Wafanyakazi wa mashirika Tanzania

Dkt. Samia Suluhu Hassan ampongeza Rais wa Namibia baada ya kuapishwa

Ushirikina wagharimu wagonjwa wa kifafa

TAGGED:BusisiKigongoMagufuliMwanza
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Nadine Vaujour: mwanamke aliyejifunza urubani ili akamtoroshe mumewe gerezani
Next Article Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version