By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kitaifa

Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili

Mwandishi Wetu
Last updated: March 23, 2025 12:08 pm
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Kampuni ya mabasi yaendayo haraka (UDART) inajiandaa kupokea mabasi mapya yanayotumia gesi asilia iliyosindikwa (CNG) kuanzia mwezi Aprili 2025.

Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa kuboresha huduma za usafiri jijini Dar es Salaam kwa kutumia nishati safi na nafuu. Ujio wa Mabasi hayo mapya unalenga kupunguza msongamano wa abiria na kuchangia katika uhifadhi wa mazingira kwa kupunguza matumizi ya mafuta ya dizeli.

Hatua hiyo ya kuingiza mabasi mapya inalenga kuyaondoa kwa awamu mabasi machakavu na yale ambayo muda wake wa kuwa barabarani yamepitwa na wakati likiwemo basi moja ambalo hivi karibuni limeonekana kwenye mitandao ya kijamii likipitisha maji sehemu yake ya kupitishia hewa (ventilation).

“Tunatarajia mabasi haya yatasaidia kuongeza ufanisi wa huduma zetu na kupunguza muda wa kusubiri kwa abiria,” Amesema msemaji wa UDART Gabriel Katanga

Mabasi yanayotumia gesi asilia (CNG) yanajulikana kwa kuwa rafiki wa mazingira, kwani hutoa kiwango kidogo cha hewa chafu ikilinganishwa na mabasi ya dizeli.

UDART imesisitiza kuwa mpango huu ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani katika kuboresha huduma za usafiri wa umma na kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.

Hatua hiyo ya kuagizwa kwa mabasi mapya katika huduma za usafiri wa mabasi yaendayo haraka inatekelezwa kufuatia kuwepo kwa changamoto ya mabasi ya awali yaliyohudumu kwa muda mrefu na kupelekea uchakavu ambapo muda wa matazamio ya kihuduma katika mabasi hayo kulingana na taarifa za mzalishaji wa Mabasi hayo ni miaka 8 hadi 10. Mabasi ya awali yaliingizwa nchini mara ya kwanza kati ya mwaka 2015-2016.

Kampuni ya Mabasi yaendayo haraka (UDART) imeeleza kuwa ujio wa mabasi mapya ni hatua muhimu kuelekea kupunguza msongamano wa abiria na kuboresha huduma kwa ujumla.

“Tunataka kuhakikisha kuwa teknolojia ya mabasi yanayotumia gesi asilia inakidhi mahitaji ya wakazi wa Dar es Salaam kabla ya kuanza operesheni rasmi za mabasi mapya mwaka huu” Kauli toka kwa Msemaji wa UDART Gabriel Katanga

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Dkt. Samia Suluhu Hassan ampongeza Rais wa Namibia baada ya kuapishwa

Watu 7 wapoteza maisha ajali ya ambulance na toyo wilayani Mafinga

Kusitishwa ufadhili wa Marekani na hatma ya Wafanyakazi wa mashirika Tanzania

RC Dar: Usalama Dar ni shwari, Ujenzi Jangwani mboini kuanza

Mbunifu wa jina la TANZANIA afariki dunia akiwa Uingereza

TAGGED:Dar es SalaamMwendokasiUDARTUsafiri
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Daraja la Magufuli kuanza kutumika Aprili 30
Next Article Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version