By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Jaji alipohukumu wasikilizaji wa kesi kumlipa fidia mtoto maskini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Visa na Mikasa

Jaji alipohukumu wasikilizaji wa kesi kumlipa fidia mtoto maskini

Mwandishi Wetu
Last updated: March 26, 2025 7:46 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Mvulana huyu mwenye miaka 13 alikamatwa akiiba Mkate dukani ambako wakati akimkimbia alipamia kona ya kabati nalo likavunjika.

Jaji aliyesikiliza shauri hili la Jinai akamuuliza Mtoto huyu kama kweli aliiba mkate na kujaribu kukimbia, Mtoto akasema ndio. Alipoulizwa kwa nini akasema aliiba mkate huo kwakuwa aliuhitaji sana! Alipoulizwa kwanini hakuununua, akajibu hakuwa na fedha na kwamba nyumbani kwao, anaishi na mama yake pekee ambaye ni mgonjwa sana na hana kazi.

Kijana huyo aliendelea kusema;

“Mimi ninafanya kazi ya kuosha magari lakini nilishindwa kwenda kutokana na hali mbaya ya mama yangu, nikajulishwa kuwa nimefukuzwa kazi”

Jaji aliyekuwa akimsikiliza kijana huyo kwa makini akamuuliza kama alifanya jitihada nyingine zozote za kuhakikisha anapata fedha, ambapo kijana huyo alimueleza Jaji kwamba aliwaomba wapita njia zaidi ya 50, hakuna aliyemsaidia ndio akaona achukue hatua hiyo ili kumuokoa mama yake na njaa licha ya kujua kwamba alichokuwa anafanya ni kosa.

Akitoa hukumu yake Jaji aliyekuwa akisikiliza shauri hilo aliwashangaza waliohudhuria kusikiliza shauri hilo kutokana na maamuzi aliyoweza kuyafanya. Jaji huyo akisoma hukumu yake alisema;

“Wizi na hasa wizi wa mkate kwa mtoto mwenye njaa ni aibu na sisi sote (tulioko katika chumba hiki cha mahakama) tunahusika na jinai hii. Kila mmoja humu Mahakamani pamoja na mimi kama sehemu ya jamii iliyoshindwa kumsaidia mtoto mwenye njaa anayo hatia na ninamhukumu (kila mmoja aliye ndani ya chumba hiki) kulipa faini ya dola kumi na hakuna yeyote atakayetoka humu ndani bila kulipa.

Aliposema hayo akatoa pochi yake na kutoa dola kumi na kuiweka mezani kisha akaanza kuorodhesha majina ya wanaolipa.

Baada ya kumalizana na wasikiliza kesi waliokuwa ndani ya mahakama kwa wakati huo, Jaji akaendelea na hukumu yake kwa kusema;

“Naliadhibu pia duka lililoshindwa kumsaidia mtoto mwenye njaa, kulipa Dola 1000 kwa kumkamata mtoto mwenye njaa na kumkabidhi kwa Polisi. Kama duka hilo lisipolipa faini hii ndani ya saa 24 ninaamuru duka hilo lifungwe. Polisi nao watalazimika kulipa Dola 1000 kwa kumkamata Mtoto mwenye njaa na kumfungulia mashitaka kumleta hapa Mahakamani” alimaliza kusoma hukumu yake

Jaji baada ya kukusanya fedha zote za faini alipiga magoti na kumkabidhi mtoto yule na kumuomba radhi kwa niaba ya jamii iliyoshindwa kumsaidia yeye na mama yake mgonjwa.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Nadine Vaujour: mwanamke aliyejifunza urubani ili akamtoroshe mumewe gerezani

Je, unawakumbuka Wasabato Masalia?

TAGGED:HukumuMkateUbinadamu
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM
Next Article Mamlaka ya Hali ya Hewa yatahadharisha ongezeko la mvua mwezi Aprili
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version