By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Mamlaka ya Hali ya Hewa yatahadharisha ongezeko la mvua mwezi Aprili
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kitaifa

Mamlaka ya Hali ya Hewa yatahadharisha ongezeko la mvua mwezi Aprili

Mwandishi Wetu
Last updated: March 26, 2025 8:25 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA) imesema kwamba katika msimu huu wa mvua za masika, kunatarajiwa ongezeko la mvua katika mwezi wa Nne mwaka huu 2025.

Akizungumza na Torchmedia ofisini kwake jijini Dar es Salaam, mchambuzi wa hali ya hewa kutoka TMA, Joyce Makwata, amesema kwamba kulingana na mifumo ya hali ya hewa, inaonyesha uwepo wa ongezeko la mvua katika mwezi wa Nne katika kipindi hiki cha mvua za masika.

Aidha, amewasisitiza wananchi kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa kila siku, ikiwemo kuchukua tahadhari mbalimbali ili kuepukana na athari za mvua zinazoweza kujitokeza.

Akizungumzia kuhusu uwepo wa joto, Makwata amesema kwamba joto litaendelea kupungua kulingana na mvua zinavyoendelea kunyesha.

Amesema kwamba uwepo wa mvua umeshusha joto kwa mkoa wa Dar es Salaam na nchi nzima kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, Makwata amesema kuwa katika maeneo mengi nchini ambayo yako karibu na misitu au miti mingi, yanatarajiwa kupata mvua nyingi ukilinganisha na maeneo mengine.

Kwa Dar es Salaam, pia Hali Iko hivyo hivyo kwa maeneo ambayo yana misitu na miti ya yanatarajiwa kupata mvua za kutosha.

Msimu wa mvua za masika ni kipindi cha mvua zinazonyesha katika maeneo mbalimbali ya tropiki, hasa katika nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, na nchi zingine za ukanda huo. Mvua hizi hutokea kila mwaka, kwa kawaida, kuanzia mwezi Machi hadi Mei, ingawa kipindi hiki kinaweza kutofautiana kidogo kulingana na eneo na mwaka.

Mvua za masika ni muhimu kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara, kwani hupatia udongo unyevu unaohitajika kwa mazao kama vile mahindi, mpunga, na maharage. Hata hivyo, mvua hizi pia zinaweza kuleta changamoto, kama vile mafuriko, uharibifu wa miundombinu, na athari nyingine za kimaumbile.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Mabasi Mapya ya Mwendokasi kuanza kupokelewa mwezi Aprili

LATRA kutilia mkazo uchunguzi wa ajali za barabarani

Serikali yazidi kuimarisha imarisha huduma za fedha ikizundua jengo la Hazina Ndogo Geita

Sita wafariki dunia ajali ya basi na lori Dodoma

TAGGED:Hali ya HewaMvuaTMA
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Jaji alipohukumu wasikilizaji wa kesi kumlipa fidia mtoto maskini
Next Article Simba waja na kaulimbiu ya HII TUNAVUKA mahususi kwa Al Masry
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version