By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Simba waja na kaulimbiu ya HII TUNAVUKA mahususi kwa Al Masry
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Michezo

Simba waja na kaulimbiu ya HII TUNAVUKA mahususi kwa Al Masry

Mwandishi Wetu
Last updated: March 26, 2025 1:49 pm
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Kikosi cha Simba Sports Club kilichotinga hatua ya robo fainali ya michuano ya CAF Confederation Cup, kinatarajiwa kuondoka nchini alfajiri ya tarehe 28 kuelekea Misri kwa mchezo wa mzunguko wa kwanza dhidi ya Al Masry.

Kwa mujibu wa msemaji wa klabu hiyo Ahmed Ally, kikosi chao kitaondoka kwa kutumia ndege ya Egypt Air ambapo wachezaji waliokuwa na Taifa Stars wataungana na timu nchini Misri. hata hivyo, mlinda mlango wao namba moja Mousa Camara na mshambuliaji Steve Desse Mukwala tayari wameshawasili nchini kujiunga na wachezaji wenzao kwa ajili ya maandalizi ya safari.”

“Kila Mwanasimba atambue kwamba pamoja na mipango tuliyonayo lakini lazima tujipange, lazima tujiandae na hasa kama timu yenyewe inatokea Misri. Ukiangalia michuano ya Afrika ilivyo utaona kwamba Misri ndio nchi iliyoingiza timu nne kwenye robo fainali, tunakwenda kucheza na Al Masry tukijua tunakwenda kucheza mechi ngumu kwelikweli lakini dhamira tuliyojiwekea ni kufuzu nusu fainali.” amesema Ahmed.

Kuhusu mechi ya marudiano ambayo itapigwa Tanzania, Ahmed amesema upo uwezekano mkubwa kwa mechi hiyo kupigwa kwenye dimba lao Uwanja wa Mkapa, baada ya kufanyiwa maboresho na wanaamini taarifa ya ukaguzi itakuwa nzuri.

“Niwatoe hofu kwamba Uwanja wa Benjamin Mkapa umeshafanyiwa ukaguzi. Bado majibu hayajatoka lakini katika mazungumzo wanasema kuna maboresho makubwa kwenye uwanja ukilinganisha na mara ya mwisho walipofanya ukaguzi hivyo kuna nafasi kubwa ya kucheza kwenye uwanja huo.”-

Kwa upande mwingine, Ahmed ametangaza kaulimbiu ya mchezo huo wa marudiano akisema

“Kaulimbiu ya mchezo dhidi la Al Masry itakuwa ni HII TUNAVUKA. Hii inamaanisha kwamba kwa misimu mitano mfululizo tunaishia robo fainali lakini safari hii tunavuka kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu.”

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

SULEIMAN MATOLA: Tunamchukulia poa poa kwakuwa ni Mtanzania

Stellenbosch kuwakosa wakali wawili ikiivaa Simba kombe la Shirikisho

Buriani Hashim Lundenga aka baba wa Miss Tanzania

Ndoa ya Yanga na Ramovic yavunjika kwa makubaliano

Serikali haitaki kutia neno sakata la “dabi” iliyoahirishwa

TAGGED:CAF CCKimataifaSimba
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Mamlaka ya Hali ya Hewa yatahadharisha ongezeko la mvua mwezi Aprili
Next Article Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version