By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Wafungwa 100 wa kike wabakwa na kuchomwa moto Goma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kimataifa

Wafungwa 100 wa kike wabakwa na kuchomwa moto Goma

Mwandishi Wetu
Last updated: February 7, 2025 12:19 pm
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

ZAIDI ya wafungwa 100 wa kike walibakwa na kisha kuchomwa moto wakiwa hai wakati wa hali ya machafuko ilipotokea baada ya wafungwa kutoroka gerezani katika mji wa Goma, nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Kwa mujibu wa ripoti mpya kutoka kwa Umoja wa Mataifa, mamia ya wafungwa walitoroka katika  gereza la Munzenze Jumatatu iliyopita, baada ya wapiganaji wa kundi la waasi la M23 kuuteka mji huo.

Ripoti hiyo inaeleza kwamba kati ya wanawake 165 na 167 walivamiwa na kunyanyaswa na wafungwa wa kiume walipovunja gereza. Wengi wa wanawake hao waliuawa baada ya wafungwa hao kuchoma moto jela.

Goma, jiji kubwa lenye zaidi ya watu milioni moja, lilitekwa na kundi la waasi la M23, linaloungwa mkono na Rwanda, lilipovamia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Machafuko yaliyoikumba Goma yalikuwa makubwa, huku miili ya watu ikiwa imetapakaa mitaani na makombora yakiripotiwa kurushwa juu ya nyumba za makazi. Picha za kivunjiko cha jela zilizochukuliwa wiki iliyopita zilionyesha watu wakikimbia kutoka jengo hilo huku moshi ukiwa unapaa angani.

Zaidi ya watu 2,000 waliuawa wakati waasi wa M23 walipokutana na wanajeshi wa Congo, huku Umoja wa Mataifa ukisema takriban watu 900 walipoteza maisha na karibu 3,000 kujeruhiwa.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Trump aiwekea vikwazo mahakama ya kimataifa ya uhalifu

Mbunifu wa jina la TANZANIA afariki dunia akiwa Uingereza

Dkt. Samia Suluhu Hassan ampongeza Rais wa Namibia baada ya kuapishwa

Nadine Vaujour: mwanamke aliyejifunza urubani ili akamtoroshe mumewe gerezani

Papa Francis afariki dunia Jumatatu ya Pasaka

TAGGED:M23Mzozo DRC
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Chimbuko la vita vya mashariki mwa DRC ni nini?
Next Article NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version