By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA

Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 8:42 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

WADAU mbalimbali katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara wameiomba serikali kwa kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali kuendeleza jitihada za kutoa elimu  kuhusu vitendo vya ukatili ya kijinsi vinayoendelea kwenye jamii yao.

Haya yamejiri wakati wa kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali za umma na binafsi kwenye manispaa hiyo kuhusu kukumbushana na masuala mbalimbali ya kisheria ikiwemo ardhi, ndoa, talaka, ukatili wa kijinsia kwa wanawake, watoto na makundi maalumu ili kila mmoja aendelee kuwa balozi wa kufikisha elimu hiyo kwa jamii.

Kikao hicho kimefanyika kwenye manispaa hiyo, kilichoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali linachojishughulisha na utoaji wa msaada wa kisheria kwa wanawake na watoto (NERIO) lililopo katika Manispaa hiyo kupitia mradi wa Sauti ya Mwanamke.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti  wa mtaa wa pentekosti, Hassan Mtiko amesema elimu hiyo ni muhimu katika jamii yao kutokana vitendo hiyo vipo kwenye jamii yao na kuziomba taasisi zinazohusika na masuala ya kisheria kuendelea kutoa ushirikiano wanapopelekewa taarifa za kuwepo kwa vitendo hivyo .

Mshiriki mwingine wa kikao hicho, Zainabu Kibunju mkazi wa kata ya mitengo ‘’Niwaombe wanawake wenzangu waache vitendo vya ukatili kwa wanaume hasa wale wanaojishughulisha na vitendo hivi kwa wanaume zao na wanaume nao waache kufanya vitendo hivi kwa wanawake zao na tunaiomba serikali, wadau elimu hii ifike zaidi katika jamii yetu’’

Mratibu wa Shirika hilo la NERIO Saidi Ismail amesema lengo la kikao hicho ni kukumbusha juu ya masuala hayo ya kisheria ili kila mmoja kwa nafasi yake aendelee kupaza sauti kuhusu vitendo hiyo vya ukatatili inavyoendelea kwa wanaume, wanawake na watoto kwenye jamii hiyo.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kwenye manispaa hiyo, Juliana Manyama amezitaka mamlaka husika kuhakikisha kuwa kesi za namna hiyo zinapofika kwao zifanyiwe kazi kwa haraka ziishe na ifike mahali vitendo hivyo viishe kabisa.

‘’Tunalo jukumu kila mmoja kwa nafasi yake tujue inafikia mahali iwe mwisho wa vitendo hivi na haviwezekani kufikiwa na taasisi moja pekee bali ni jukumu la kila mtu’’amesema Manyama

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Mikindani kutumia bilioni 33 mwaka ujao wa kifedha

Wanafamilia washikiliwa na Polisi wakituhumiwa kuua baba yao mzazi

UCHUNGUZI WA VURUGU SHULE YA SEKONDARI YA GEITA, WANAFUNZI 71 WACHUKULIWA HATUA

Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao

Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi

TAGGED:JinsiaMikindaniMtwaraNGOUkatili
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Wafungwa 100 wa kike wabakwa na kuchomwa moto Goma
Next Article Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version