By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Mikindani kutumia bilioni 33 mwaka ujao wa kifedha
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Mikindani kutumia bilioni 33 mwaka ujao wa kifedha

Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 12:16 pm
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara limepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya Sh bilioni 33,544,971,406 ambapo manispaa hiyo imekisia kukusanya na kutumia fedha hizo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Akizungumza wakati wa kikao cha baraza la madiwani hao, Meya wa manispaa hiyo Shadida Ndile amesema madiwani hao waende wakawahamasishe wananchi wao wakakusanye fedha ili waweze kuyatekeleza yale wanayotamani kuyaona yanayoendelea kwenye maeneo yao.

Aidha amewasisitiza madiwani hao wazingatie vipaumbele ambavyo kila kata vimeweka “Naamini kata zote tumezigusa kwenye miradi ya maendeleo na dhamira yetu ni kuendelea kugusa miradi ya maendeleo ili kipunguza changamoto kwa wananchi”amesema Ndile

Ameongeza kuwa, ” Twende tukakusanye tukirudi tutaangalia kila kata kipaumbele chake upande wa elimu kipi, afya, mazingira kipi tutakwenda kuyafanya lakini haya yote yanawezekana endapo tutakuwa na fedha za kutosha tutazoweza kwenda kutekeleza majukumu haya”

Hata hivyo amewashukuru wataalamu katika manispaa hiyo kwa kuchakata vizuri mpango huo wa bajeti uliyopitishwa na madiwani hao hivyo ni imani yake kuwa baina ya timu hizi mbili wakienda kushirikiana wataenda kupunguza baadhi ya changamoto.

Diwani wa Kata ya Naliendele, Masudi Dali kupitia kikao hicho ameunga mkono bajeti hiyo na kwamba madiwani hao waendelee na ukusanyaji mapato katika maeneo yao ili waweze kufikia malengo yanayokusudiwa.

Diwani wa Kata ya Shangani, Abuu Mohamed ameliomba baraza hilo kuangalia suala la kuwapatia mikataba wafanyabiashara wa soko la kiyangu (Sokosela) lililopo kwenye manispaa hiyo ili waweze kufanya kazi zao kwa uhakika.

Meya wa Manispaa Mtwara Mikindani, Shadida Ndile

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

Wanafamilia washikiliwa na Polisi wakituhumiwa kuua baba yao mzazi

Hakikisheni elimu ya malezi inaifikia jamii kikamilifu – Theresia Ngonyani

Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi

NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA

TAGGED:MadiwaniMtwaraMtwara Mikindani
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Tanzania yatwaa tuzo ya uimarishaji usalama barabarani kimataifa
Next Article Mahakama ya Rufaa yabariki adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa SSP Bageni
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version