By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Mahakama ya Rufaa yabariki adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa SSP Bageni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kitaifa

Mahakama ya Rufaa yabariki adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa SSP Bageni

Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 1:57 pm
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

Shauri la mapitio ya hukumu ya kunyongwa iliyokuwa imetolewa kwa SSP Christopher Bageni, limetamatika kwa mahakama ya rufaa nchini kuafiki hukumu hiyo ambayo ilitolewa na mahakama hiyo hiyo miaka 9 iliyopita.

Uamuzi huo ulitolewa februari 19, 2025 na Jani Jaji Stellah Mugasha amegonga nyundo na kwa uamuzi huo SSP Bageni sasa hawezi tena kukata rufaa tena kwa sababu hukumu ya jana imetolewa baada ya ni mapitio (review) ya hukumu iliyotolewa na Mahakama hiyo September 16, 2016, ambapo alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Benard Luanda.

Kwa wasiokumbuka Bageni alikua Mkuu wa Upelelezi wilaya ya Kinondoni. Mwaka 2006 yeye na wenzie wakiongozwa na aliyekua Kaimu RPC Dar, Abdalah Zombe, walituhumiwa kupanga njama za kuwauwa wafanyabiashara watatu wa Morogoro. Zombe anadaiwa ndiye aliyeongoza wenzie kwenye mpango huo, baada ya kujulishwa kuwa wana madini na fedha kiasi cha shilingi milioni 200.

Walikamata gari waliyokua wameikodi. Wakamuongoza dereva hadi msitu wa Mabwepande. Wakapora madini pamoja na fedha zote walizokua nazo. Kisha wakawafunga vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi. Kisha wakawapiga risasi za kisogoni na kuwauwa wote akiwemo dereva wa taxi waliyemkodisha.

Kesho yake Zombe akaita media na kusema wameua majambazi yaliyokua yanarushiana risasi na Polisi. Mhe. Rais Kikwete akaunda tume ya Jaji Kipenka kuchunguza. Ikabainika hawakuwa majambazi. Kilichouma zaidi walikua ndugu wa familia moja. Mama mmoja alipoteza wanae watatu. Watoto wa familia 4 wakapoteza baba zao, na wake wanne wakawa wajane kwa tamaa za polisi.

Zombe alifanikiwa “kuchomoka” kwenye kesi hii baada ya kusota rumande kwa miaka kadhaa. Lakini Bageni alipatikana na hatia akahukumiwa kunyongwa. Akakata rufaa ikafeli, akaomba review ya kesi, na maamuzi yakasomwa jana kuwa anyongwe hadi kufa

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Biteko akemea ubabe Tanesco, ataka hatua

Hongera Dkt. Samia Suluhu Hassan, umeweza, tusonge mbele

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

RC Dar: Usalama Dar ni shwari, Ujenzi Jangwani mboini kuanza

Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Mikindani kutumia bilioni 33 mwaka ujao wa kifedha
Next Article Mkasa wa Billionaire Eric Mandala wa DRC kunaswa na madawa ya kulevya
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version