By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Hongera Dkt. Samia Suluhu Hassan, umeweza, tusonge mbele
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kitaifa

Hongera Dkt. Samia Suluhu Hassan, umeweza, tusonge mbele

Mwandishi Wetu
Last updated: March 20, 2025 11:37 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

RAIS Samia Suluhu Hassan leo anatimiza miaka minne ya uongozi wake wa Awamu ya Sita tangu alipoapishwa Machi 19, 2021 kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kifo cha Dk John Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021.

Wakati anahutubia Bunge la Tanzania mwezi mmoja baadaye jijini Dodoma, Rais Samia aliahidi kwamba ataendeleza mema yaliyofanywa na mtangulizi wake, Dk Magufuli.

Pia, alisema atasimamia na kuendeleza mengine ambayo uongozi wake wa Awamu ya Sita utakuwa umeyaanzisha.

Leo hii tunapoadhimisha miaka minne ya uongozi wake katika nafasi hii ya juu ya madaraka ya nchi, hakuna shaka yoyote, Rais Samia ameyaishi maneno yake.

Ametekeleza aliyoahidi na amefanya makubwa zaidi kwa ustawi wa nchi.

Toleo la leo limebeba sauti nyingi za Watanzania kuhusu mambo yaliyofanywa na Rais Samia ambayo yameleta mafanikio makubwa kwa maendeleo ya Tanzania na watu wake kuanzia katika huduma za jamii hadi katika diplomasia ya uchumi.

Chini ya Rais Samia, serikali imeboresha huduma za jamii zikiwamo za afya, elimu, maji na kupunguza umasikini, ambako kwa mujibu wake umasikini umepunguzwa kwa kiwango cha asilimia 26 kutoka katika kiwango kilichokuwapo mwaka 2015.

Kwa mfano, katika sekta ya afya, serikali imeongeza miundombinu, vifaa tiba na upatikanaji wa dawa.

Kwenye elimu, ukiacha majengo mazuri ya madarasa na maabara yaliyojengwa kote nchini, mikopo na wanufaika wa elimu ya juu wameongezeka, usajili katika shule za msingi na sekondari umeongezeka na udahili umeongezeka katika vyuo vikuu.

Katika sekta ya maji, Tanzania imefikia mafanikio ya Malengo Endelevu ya Maendeleo (SDGs), ikitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2020 – 2025 ambayo sasa imefikisha maji vijijini kwa asilimia 80 na mijini asilimia 90 na wakati malengo ya ilani ni asilimia 85 na 95 mtawalia.

Ni imani yetu kuwa kazi hii kubwa iliyofanywa na Rais Samia katika miaka minne ya uongozi wake inaakisi maono yake chini ya falsafa yake ya ‘4R’ ya Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga upya Taifa.

Kubwa ni Watanzania kuendelea kumuunga mkono, Rais Samia na serikali yake ili aendelee kuwapatia maendeleo zaidi.

Na hapa ni lazima kusisitiza amani na utulivu udumishwe nchini ili haya yanayofanywa sasa yaendelea kutekelezwa. Rais Samia amethubutu, ameweza na anasonga mbele. Kazi Iendelee!

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Mahakama ya Rufaa yabariki adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa SSP Bageni

Mkuu wa Wilaya Ubungo ateuliwa Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Je, unawakumbuka Wasabato Masalia?

Kamati ya Bunge yakoshwa na utendaji TPA

Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Dar msisubiri mwishoni kujiandikisha daftari la wapigakura
Next Article Dkt. Samia Suluhu Hassan ampongeza Rais wa Namibia baada ya kuapishwa
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version