By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao

Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 9:02 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

MTWARA: JAMII katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara hususani wanaume wanaoishi na wanawake wenye fani mbalimbali ikiwemo ufundi chuma, wameshauri kuwaruhusu wanawake hao waendeleze fani hiyo ili waweze kuwa mafundi kama ilivyokuwa mafundi wengine.

Akizungumza mkoani Mtwara wakati wa mafunzo ya wiki mbili yanayoendelea kwa vijana wa fani hiyo kuhusu masuala ya ufundi chuma, Mwenzeshaji wa mafunzo hayo Omari Mohamed amesema baadhi ya wanawake hao wengi wao wamekuwa wakipitia changamoto hiyo na kupelekea kushindwa kuendeleza fani hiyo.

Mafunzo hayo yamefanyika katika manispaa hiyo na kukutanisha vijana wa kike na wa kiume wa fani hiyo yaliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na masuala mbalimbali ya sanaa na utamaduni la ADEA lililopo kwenye manispaa hiyo, yanayofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

‘’Unakuta mwanafunzi wa kike anapitia haya mafunzo mwisho wa siku anashindwa kuendeleza fani anabaki nyumbani na wengi wao wanashawishiwa, sasa sijajua kama na wanaume au lah……unakuta mwanamke mwingine hii kazi anaitaka kwa kuwa ndiyo fani aliyochangua na kuolewa anataka kwahiyo changamoto inakuja hapo’’amesema Mohamed

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo la ADEA, Saidi Chilumba amesema fani hiyo imekuwa ngumu kwasababu baadhi ya jamii inaamini kuwa fani hiyo ni ya watoto wa kiume pekee lakini mafunzo hayo yameshirikisha vijana wa jinsia zote ambao wamejifunza kwa nadharia pamoja na vitendo kwa kutengeneza vitu mbalimbali vya chuma.

Hata hivyo amewataka vijana hao kubuni bidhaa zitazokuwa na uwezo wa kuwauzia wananchi wa kawaida ambavyo ni vidogo vidogo vinavyohatajika na jamii ila hawajuwi wapi vinapatikana hivyo ni fursa kubwa kwao na maamuzi ya kushirikisha vijana hao wa kike ni kutokana vile wanapata mafunzo lakini hawaonekani mitaani wakiendelea fani hiyo.

Baadhi ya vijana hao wa kike akiwemo Asfa Rashidi mkazi wa magomeni kwenye manispa hiyo ‘’Sisi watoto wa kike kwa hii fani tunapokuja mtaani tatizo jamii inatukatisha tamaa, tunaambiwa mnafanyaje hizi kazi za watoto wa kiume au unatokaje nyumbani mtoto wa kike kutwa mzima unaenda kushinda kijiweni, basi unasema ngoja niachane tu na hii kazi’’

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Hakikisheni elimu ya malezi inaifikia jamii kikamilifu – Theresia Ngonyani

Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2

Dk. Kalemani – Sauti ya Wanawake ni Sauti ya Mungu

DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka

NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA

TAGGED:UfundiWanawake
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article NGO ZISHIRIKISHWE MAPAMBANO YA UKATILI WA KIJINSIA
Next Article Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version