By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka

Mwandishi Wetu
Last updated: February 22, 2025 11:17 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara mkoani Mtwara limepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya Sh bilioni 32,517,899,127 ambapo halmashauri hiyo imekisia kukusanya na kutumia fedha hizo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Hayo yamejiri wakati wa kikao hicho cha baraza hilo la madiwani hao kilichofanyika kwenye halmashauri hiyo.

Akichangia mada katika kikao, Diwani wa Viti Maalumu, Mariam Lilepe ameipongeza rasimu hiyo ya bajeti na kuhusu kutilia mkazo suala la ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao mbalimbali yanayozalishwa kwenye halmashauri ili kukuza pato la halmashauri.

Hata hivyo amesisitiza suala la ujenzi wa eneo la kupaki magari (Parking) kwenye halmashauri hali itayochangia tija zaidi kwenye ukusanyaji wa mapato hayo.

Diwani wa Kata ya Mayanga, Arif Premji ameunga mkono suala hilo la ujenzi wa ghala ambapo ameliomba baraza hilo kuwa, ujenzi huo ufanyike kwenye kata hiyo kwasababu ni moja ya kata inayochangia pato la halmashauri.

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Abdallah Mwaipaya amepongeza mchakato mzima wa rasimu hiyo ya bajeti kwasababu imezingatia maeneo yote muhimu ikiwemo sekta ya elimu na mengine.

Mbali na hilo Mkuu huyo wa wilaya amesisitiza suala la utoaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kuwa itolewe kabla ya Februari 2025 kumalizika.

“Hakikisheni mnatoa mikopo hii kabla mwezi huu wa 2/2025 haujaisha, kwasababu pesa tayari ipo”amemsisitiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Dk. Kalemani – Sauti ya Wanawake ni Sauti ya Mungu

Wanafamilia washikiliwa na Polisi wakituhumiwa kuua baba yao mzazi

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao

Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2

TAGGED:BajetiMikopoMtwaraVijanaWalemavuWanawake
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Mkasa wa Billionaire Eric Mandala wa DRC kunaswa na madawa ya kulevya
Next Article Mhe. Kanyasu atimiza ahadi ya pikipiki kwa wanahabari Geita
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version