By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara limepitisha makadirio ya bajeti ya Sh bilioni 40.239 kwa mwaka wa fedha 2025/2026

Mwandishi Wetu
Last updated: February 20, 2025 9:12 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara limepitisha makadirio ya bajeti ya Sh bilioni 40.239 kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Hayo yamejiri leo wakati wa kikao maalum cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kuhusu makisio ya mpango wa bajeti kwa mwaka huo wa fedha 2025/2026, kilichofanyika kwenye halmashauri hiyo.

Akiwasilisha bajeti hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo ya  Wilaya ya Tandahimba, Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu wilayani humo David Sinyanya alisema katika bajeti hiyo ni kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ikiwemo Sh bilioni 7.3 mapato ya ndani, Sh bilioni 24.9 ruzuku ya mishahara, Sh bilioni 5.06 wafadhili na Sh bilioni 2.8 matumizi mengineyo (OC).

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji DCI Mariam Mwanzalima alisema kila mwaka wa fedha wamekuwa na jitihada ya kuhakikisha wanakamilisha miradi ya nyuma ili waweze kwenda na miradi mipya na ili waweze kufikia malengo ya makusanyo hayo ni imani yake kwa ushirikiano na wananchi wake wataweza kufikia malengo hayo.

Hata hivyo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 halmashauri ilikisia kukusanya Sh bilioni 6.1 lakini hadi kufikia Disemba 2024 ilikusanya Sh bilioni 6.9 sawa na asilimia  112.

Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Kanali Michael Mntenjele kupitia baraza hilo amesisitiza suala la hali ya ulinzi na usalama katika wilaya hiyo kuwa ni salama kwani vikosi vyao vinaendelea na majukumu yake kama kawaida.

“Ila na sisi wananchi tunapaswa kutimiza majukumu yetu ya ulinzi shirikishi ili kuendelea kudumisha hali ya amani katika maeneo yetu”alisema Mntenjele

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Baisa Baisa ameendelea kuwaomba madiwani hao pamoja na watendaji wa halmashauri kwa ujumla kuwa, waendelee kushirikiana katika suala zima la ukusanyaji wa mapato ili waweze kufikia malengo husika ya bajeti hiyo ya mwaka 2025/2026 kama ilivyokuwa bajeti za miaka iliyopita.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao

Chato yakabiliwa na upungufu wa madawati shule za msingi

UCHUNGUZI WA VURUGU SHULE YA SEKONDARI YA GEITA, WANAFUNZI 71 WACHUKULIWA HATUA

Mhe. Kanyasu atimiza ahadi ya pikipiki kwa wanahabari Geita

TAGGED:Bajeti
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Wapeni wake zenu nafasi ya kuendeleza ujuzi wao
Next Article Hakikisheni elimu ya malezi inaifikia jamii kikamilifu – Theresia Ngonyani
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version