By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Trump aiwekea vikwazo mahakama ya kimataifa ya uhalifu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Kimataifa

Trump aiwekea vikwazo mahakama ya kimataifa ya uhalifu

Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu
Mwandishi Wetu
Last updated: February 7, 2025 9:20 am
Mwandishi Wetu
3 months ago
Share
SHARE

Rais Donald Trump ametia saini amri ya utendaji inayoiwekea vikwazo Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, akiituhumu kwa “vitendo vinavyokiuka sheria na visivyo na msingi vinavyoilenga Marekani na mshirika wetu wa karibu Israel”.

Hatua hiyo inaiwekea vikwazo vya kifedha na visa kwa watu binafsi na familia zao wanaosaidia katika uchunguzi wa ICC wa raia au washirika wa Marekani.

Trump alitia saini hatua hiyo wakati Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alipokuwa akizuru Washington.

Novemba mwaka jana, ICC ilitoa hati ya kukamatwa kwa Netanyahu kwa tuhuma za uhalifu wa kivita huko Gaza, jambo ambalo Israel inakanusha. ICC pia ilitoa kibali cha kukamatwa kwa kamanda wa Hamas.

Amri ya utendaji ya Trump ilisema hatua za hivi majuzi za ICC “ziliweka historia ya hatari” ambayo inahatarisha Wamarekani kwa kuwaweka kwenye “unyanyasaji na uwezekano wa kukamatwa”.

“Tabia hii mbovu nayo inatishia kukiuka uhuru wa Marekani na inadhoofisha kazi muhimu ya usalama wa kitaifa na sera ya kigeni ya serikali ya Marekani na washirika wetu, ikiwa ni pamoja na Israel,” amri hiyo ilisema.

Marekani si mwanachama wa ICC na mara kwa mara imekataa mamlaka yoyote ya chombo hicho juu ya maafisa wa Marekani au raia.

Chanzo: BBC Swahili

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

Je wajua kwamba Pepsi iliwahi kuwaokoa washindani wake CocaCola dhidi ya wizi wa kibiashara?

MZOZO DRC: Afrika Kusini yaapa kurejesha wanajeshi wake nyumbani wakiwa salama

Nadine Vaujour: mwanamke aliyejifunza urubani ili akamtoroshe mumewe gerezani

Mbunifu wa jina la TANZANIA afariki dunia akiwa Uingereza

Wafungwa 100 wa kike wabakwa na kuchomwa moto Goma

TAGGED:Donald TrumpICCIsraelMarekaniVikwazo
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Ndoa ya Yanga na Ramovic yavunjika kwa makubaliano
Next Article Kusitishwa ufadhili wa Marekani na hatma ya Wafanyakazi wa mashirika Tanzania
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version