By using this site, you agree to the Privacy Policy and Terms of Use.
Accept
YanayojiriYanayojiriYanayojiri
  • Home
  • Home
    • Home 2
    • Home 3Hot
    • Home 4
    • Home 5New
  • Posts
    • Post Layouts
    • Gallery Layouts
    • Video Layouts
    • Audio Layouts
    • Post Sidebar
    • Review
      • User Rating
    • Content Features
    • Table of Contents
  • Pages
    • Search Page
    • 404 Page
Reading: Wananchi Mtwara wawaelimishwe kuhusu uchaguzi mkuu – Padri Kitima
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
YanayojiriYanayojiri
Font ResizerAa
  • Categories
  • Home
    • Home 1
    • Home 2
    • Home 3
    • Home 4
    • Home 5
  • More Foxiz
    • Login
    • Contact
    • Blog
    • Buy Theme
  • Demos
  • Categories
  • Bookmarks
  • More Foxiz
    • Sitemap
Have an existing account? Sign In
Follow US
  • Advertise
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Mikoani

Wananchi Mtwara wawaelimishwe kuhusu uchaguzi mkuu – Padri Kitima

Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Padre Charles Kitima
Mwandishi Wetu
Last updated: March 20, 2025 11:24 am
Mwandishi Wetu
2 months ago
Share
SHARE

Viongozi wa dini mbalimbali (Interfaith) mkoani Mtwara wametakiwa kuendelea kuwaelimisha wananchi katika masuala mbalimbali ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2025 hasa suala la amani na utulivu.

Hayo yamejiri wakati wa mafunzo ya siku mbili kwa viongozi wa dini mbalimbali mkoani humo kuhusu elimu ya uraia yanayoendeshwa na Sekretarieti ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) yaliyofanyika kwenye Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Padre Charles Kitima amesema viongozi hao dini wakati wakiendelea na shughuli za kuabudu wasiache kuwaelimisha wananchi hao masuala ya kisiasa ila jambo la msingi waangalie mazingira ya kutoa elimu hiyo.

“Ni haki yako kiongozi wa dini kuwaambia wananchi masuala ya siasa ila angalieni namna ya kuongelea masuala haya ili waweze kukuelewa na waweze kujiandaa na mambo ya uchaguzi, tuwape watu elimu ya uchaguzi wenye amani na utulivu,”amesema Kitima

Aidha lengo la mafunzo hayo ni kuwapatia viongozi hao wa dini baadhi ya mambo muhimu wanayopaswa kuzingatia katika uongozi ikiwemo maarifa, uelewa juu ya masuala ya kuongoza nchi, kujipatia nyenzo za kutawala na kuongoza pamoja na namna ya kufata taratibu.

“Viongozi wa kisiasa wameumbwa kuwatumikia wanadamu wote waliyoumbwa kwa mfano wa Mwenyezi Mungu, wanaojituma, wanaojielewa na kiongozi wa kisiasa ni agizo la Mwenyezi Mungu hivyo twendeni tukatoe elimu ya masuala haya ya uchaguzi kikamilifu ili wananchi wapate uelewa “amesisitiza Kitima.

Amesema wanahitaji elimu ya uraia nchini iwe endelevu katika jamii hivyo viongozi hao wa dini waje na mkakati wa kuona elimu hiyo kuwa ni sehemu ya wajibu wao ili mwisho wa siku wawe na Taifa lenye uadilifu.

Hata hivyo kupitia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameendelea kuwakumbusha viongozi hao kuwa hawapaswi kufungamana na chama chochote kike cha siasa pia wawaambie wananchi wajitokeze kupiga kura wakati uchaguzi huo utakapofika hivyo wanao wajibu wa kujiandaa kikamilifu na kushiriki moja kwa moja katika zoezi hilo.

Mkurugenzi wa Miradi wa TEC, Padre Chrisantus Ndaga amewataka viongozi hao wanapojiandaa na uchaguzi mkuu huo kuhakikisha wanaendelea kujenga uelewa zaidi hasa katika masuala hayo ya uchaguzi ili kuwafanya watu wafanye maamuzi sahihi katika ushiriki wao kwenye nafasi mbalimbali za uongozi.

Viongozi hao wa dini waliyopatiwa mafunzo hayo wakiwemo kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) mkoani Mtwara, Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) pamoja na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

You Might Also Like

DC Mwaipaya aagiza mikopo ya vijana, wanawake wenye ulemavu kutolewa haraka

Hamasisheni Uwekezaji Mtwara – Dk. Hussein

Madiwani Tandahimba wapitisha bajeti ya bilioni 40.2

Polisi Simiyu watoa ufafanuzi gari lao kubeba wanachama wa CCM

Rais Samia aagiza madereva wanaosababisha vifo kufutiwa kabisa leseni zao

TAGGED:ElimuMtwaraUchaguzi
Share This Article
Facebook Email Print
Previous Article Serikali haitaki kutia neno sakata la “dabi” iliyoahirishwa
Next Article Halotel wazindua huduma kukabili matapeli mitandaoni
Leave a Comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

UNGANA NASI

Unaweza kuwa sehemu ya familia hii kwa kuchangia kuleta taarifa za yanayojiri eneo lako, kuchangia makala, kushirikisha uzoefu wako kwa kutoa maoni na hata kuuliza ili kufahamu zaidi. Kujiunga nasi, tafadhali tuandikie kupitia karibu@yanayojiri.com  

© Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Join Us!
Subscribe to our newsletter and never miss our latest news, podcasts etc..
Zero spam, Unsubscribe at any time.
Go to mobile version